Showing posts with label tukio. Show all posts
Showing posts with label tukio. Show all posts

Saturday, October 1, 2016

Diamond amuombea kura Alikiba kwenye tuzo za MTV EMA 2016

Kuna uwezekano mkubwa kukawa hakuna bifu kati ya Alikiba na Diamond lakini wapo wachache wanaokuza hilo jambo kwa maslahi yao binafsi. Diamond ameonekana kulipa fadhila kwa Alikiba baada ya kumuombea mashabiki wampigie kura kwenye tuzo ya MTV EMA 2016 akiwa msanii pekee kutoka Afrika Mashariki anayewania tuzo hiyo



Kiba atachuana na wasanii wengine wakiwemo Wizkid na Olamide wa Nigeria na Black Coffee na Cassper Nyovest wa Afrika Kusini huku mshindi katika hatua ya kwanza ataendelea kwenda kuwania kipengele cha Worldwide Act: Africa/India ambacho mwaka jana alishinda Diamond Platnumz.
Akiongea kwenye kipindi cha D’Wikend Chatshow cha Clouds TV, hitmaker huyo wa Salome amesema, “Nimesikia Alikiba amechaguliwa kwenye tuzo za MTV EMA. Tufute zile zama za kusema kwasababu wewe unam-support Diamond ndio huwezi kumpigia kura Alikiba. Akikosa tuzo hiyo haiji kabisa Tanzania na itaonekana watanzania wote tumeikosa. Kwahiyo tuhakikishe tuna VOTE ili tuirudishe tuzo hiyo nyumbani.”
Alikiba aliwahi kusema kama hivyo mwezi Juni, mwaka huu kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa TV alipowataka mashabiki wampigie kura Diamond kwenye tuzo za BET.

Saturday, September 10, 2016

Dully Sykes aongea hiki baada ya Nuh Mziwanda kudai kuibiwa idea ya wimbo ‘Inde’

Baada ya mkali wa wimbo ‘Jike Shupa’ Nuh Mziwanda kudai kuibiwa idea ya wimbo ‘Inde’, Dully Sykes amefunguka na kuzungumzia sakata hilo.



Hivi karibuni Nuh alidai katika maktaba yake ana wimbo ambao unaitwa ‘Inde’ lakini atashindwa kuutoa baada ya kusikia ‘Inde’ ya Dully mtaani huku akimtuhumu producer wake kula njama na Dully Sykes na kutoa idea ya wimbo huo.
Akiongea katika kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa hii, Dully Sykes amesema idea ya wimbo ‘Inde’ haikuwa yake, alipewa na Harmonize na yeye kuiboresha zaidi.
“Idea ya ‘Inde’ siyo yangu,” alisema Dully Sykes. “idea ya ‘Inde’ niya Harmonize, nimemkuta nayo mimi nilikuwa sina hata idea hiyo yakusema niimbe ‘Inde’, wala sijui kuhusu maswala ya Inde,”
Alivyoulizwa Harmonize kuhusu idea ya wimbo ‘Inde’ alisema, “Labda mimi nizungumze kitu kimoja, unajua mimi ni msanii mchanga sana, kwanza sina hata miaka 3, siyo kwamba najua sana vitu vingi, lakini vichache navyovijua huwa napenda sana kuweka wazi ili na watu wavijue. Unajua mtu kama Dully Sykes mimi nimeanza kumsikia toka nipo kijijini huko, kila siku anatoa nyimbo, ana hit kibao. Sometime vijana tukiwa tunatafuta angle tutafute angle nzuri kwa sababu kuja kumwambia brother Dully kachua wimbo wako au kaiba, unamvunjia heshima, unaukosea heshima muziki wa bongofleva pia, kwa sababu unavyomzungumzia brother Dully unauzungumzia muziki wa bongofleva, so kumwambia brother Dully wimbo uliotoa na mimi na wimbo wangu wa miaka miwili sijautoa ni kumkosea heshima,” alisema Harmonize.
Wimbo ‘Inde’ wa Dully Sykes unafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya radio na rudinga huku YouTube ukiwa na views milioni moja kwa kipindi cha mwezi mmoja toka utoke.

Wema Sepetu amvutia wire Soudy Brown ‘Man Fongo sio mtu wa kubishana na mama yangu’

Baada ya kusambaa audio katika mitandao ya kijamii ambazo mama Wema anasikika akimpandishia mtangazaji wa Clouds FM, Soudy Brown, Wema Sepetu amemvutia wire mtangazaji huyo akimtaka kuacha kumzungumzia mama yake katika mambo ambayo hayaeleweki.



Chanzo mgogoro huo mkubwa kati ya Wema Sepetu dhidi ya Christian Bella na Man Fongo kwa pamoja, unahusiana na masuala ya show ambazo ‘design’ wamezungukana na mama ameingilia kati!.
Hivyo Soudy kama kawaida yake aliongea na Man Fongo kujua upande wake wa mkasa huo, lakini alijikuta katika wakati mgumu alivyoamua kumpigia mama Wema ili apate chochote kitu kuhusu ubuyu huyo.
Ijumaa hii Wema Sepetu kupitia kipindi cha U Head, aliamua kumtolea uvivu mtangazaji huyo akimtaka kutomwingiza mama yake katika mambo alioyaita yakijinga.
“Soudy hebu acha kumweka mama kwenye hayo mambo, nakuomba mama yangu sijamuweka kwenye hayo mambo, mama yangu ni mtu mzima namweshimu, nakuomba achana na mambo hayo sijui kumpigia simu, sijui maswala ya Man Fongo, nani anamjua Man Fongo?,” aliuliza Wema. “Man Fongo kweli yule wakukaa kubishana na mama yangu, kwa nini mnamrekodi mama yangu hivyo, mimi sipendi,”

Friday, September 9, 2016

Mechi itakuwa ngumu zaidi bila Aguero – Mourinho

Kocha wa klabu ya Man United Jose Mourinho amesema kuwa mechi ya leo dhidi ya mahasimu wao Man City itakuwa ngumu licha ya Sergio Aguero kukosekana.

Thursday, September 8, 2016

NEW VIDEO: G-Lax - SIO KOLOLO

Msanii Mkali chipukizi ameachia video yake mpya wimbo unaitwa #SIOKOLOLO unaweza kuiangalia hapa


    BOFYA LINK HII HAPA CHINI !
     https://www.youtube.com/watch?v=eHAoVr3mQMo

Saturday, September 3, 2016

Ycee amesema haya kwa wasanii bongo na Africa kiujumla

Rapper na muimbaji Nigeria, Ycee amedai kuwa si rahisi kwa wasanii wa Tanzania na hata wa nchi zingine kutoboa Afrika nzima bila kufanya collabo na wasanii wa nchi zingine.

Ycee akiwa na watangazaji wa kipindi cha The Cruise cha East Africa Radio

Baada ya kumuuliza ni wasanii gani wa Tanzania wanafahamika Nigeria na kuwataja Diamod, Alikiba, Vanessa Mdee na Navy Kenzo, nilimuomba atoe ushauri kwa wasanii wengine wanaofanya vizuri lakini hawafahamiki nje ya Afrika Mashariki, Ycee alisema collabo ndio jibu.
Alijitolea mfano mwenyewe kuwa baada ya kuwa kimya na baadaye kurejea kwenye muziki, ili kufahamika kwa wengi ilimlazimu kumshirikisha mtu anayejulikana tayari.
“Nadhani ni kile kile, kama unataka kupenya kwenye soko la Marekani kwa mfano, bila shaka itabidi ufanye kazi na msanii wa Marekani. Kama wamarekani wanatafuta muziki na kuona jina la mtu wasiyemjua ni rahisi kulipita,” alisema.

Wednesday, June 8, 2016

Queen Darleen asema alikuwa mfanyakazi ndani ya ‘WCB’ kabla ya kusaini kama msanii

Msanii wa muziki ambaye pia ni dada wa staa wa muziki Diamond Platnumz, Queen Darleen baada ya kusaini WCB hivi karibuni, amefunguka na kueleza jinsi alivyokuwa ananufaika na mafanikio ya kaka yake.































Akizungumza na Bongo5 Jumatatu hii, Queen Darleen amesema alikuwa ni mfanyakazi wa kawaida ndani ya WCB na alikuwa akilipwa mshahara kama wafanyakazi wengine.
“Kabla ya kusaini WCB maisha yangu yalikuwa yameshabadilika,” alisema Darleen “CEO tayari alikuwa ameshanibadilishia maisha yangu, nilikuwa nafanya kazi mbalimbali ndani ya WCB na nilikuwa nalipwa, kama zile behind the scenes nilikuwa nazisimamia mimi,”
Muimbaji huyo amezungumzia hatua ya kusaini ‘WCB’.
“WCB ni label ambayo inafanya poa kwa sasa, kwa hiyo kufanya kazi chini ya ‘WCB’ ina maana kwamba muziki wangu sasa unaenda katika level nyingine, hii ni hatua nzuri, tuombe Mungu mambo yaende vizuri, muziki wangu utafika mbali zaidi, kwa hiyo mashabiki wakae mkao wa kula kwa ajili ya vitu vipya na vizuri, nini ndiye Queen ‘WCB’,” alisema Darleen.

KISHEY PLATNUMZ!

Rich Mavoko adai kuwa kuna msanii mkubwa wa Bongo alimuambia asisaini WCB

RICH MAVOKO
Sio watu wote waliofurahia Rich Mavoko kusainiwa chini ya label ya WCB, ikiwemo wasanii wengine wakubwa wa Bongo Fleva.
Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo, Mavoko amedai kuwa kuna msanii alimkataza kusainiwa chini ya label hiyo inayomilikiwa na Diamond Platnumz baada ya taarifa za yeye kusainiwa kwenye label hiyo kutoka.
WCB WASAFI           

“Sijawahi kusema hili ila ukweli ni kwamba wakati nataka kwenda WCB kuna msanii mkubwa alinitumia ujumbe na kuniambia Rich Mavoko unakwendaje kusimamiwa kazi zako na Diamond Platnumz ” Mavoko alifunguka. “Kiukweli aliniumiza sana ila nilimjibu kwa roho moja kuwa brother wewe hujui mimi nimetoka wapi na nakwenda wapi hivyo huwezi kujua hata hili litakujae kwangu.”

Rich Mavoko tayari ameachia wimbo wa kwanza akiwa chini ya label hiyo, Ibaki Story ambayo inazidi kufanya vizuri kwenye media mbali mbali vikiwemo TV na RADIOS.

KISHEY PLATNUMZ!

KENYA YAKOSA UMEME TAKRIBANI SIKU NNE KISA NI.....


Kampuni ya kuzalisha umeme nchini Kenya, KENGEN imetuma taarifa kwa vyombo vya habari ikiomba radhi kwa ukosefu wa umeme Kwa hapo jana.
Hilo sio jambo geni.
Mara kwa mara umeme hupotea nchini Kenya kwa sababu moja au nyengine, sawa tu na mataifa yote barani Afrika
Hata hivyo sababu walioitoa KENGEN kwa ukosefu huo wa umeme Kwa takriban saa nne kote nchini humo ndio imewaacha wengi wamepigwa na butwaa !

Nyani.


Amini usiamini, KENGEN imempata nyani mmoja katika eneo maalum lenye 'swichi' hiyo katika mtambo wa kuzalisha umeme ulioko kwenye bwawa kuu la Gitaru Mashariki mwa Kenya.
Sasa kampuni hiyo inasema huenda nyani huyo ndiye aliyezima umeme kote nchini Kenya !
Kengen inasema kuwa huenda nyani huyo aliangukia mashine hiyo ndogo na ''kusababisha hitilafu ya takriban megawati 180 za umeme ambao ndio uliosababisha ukosefu wa umeme kote nchini Kenya.''

 Kwa takriban saa nne taarifa hiyo ilielezea.

Tumbili huyo alinusurika na sasa amechukuliwa na shirika la huduma kwa wanyama pori KWS ilikupokea matibabu.
"mitambo ya kuzalisha umeme kote nchini Kenya huwa imezingirwa na nyaya za umeme ilikuwazuia wanyama wa porini kuingia humo na kusababisha madhara kama hayo ya jana , taarifa hiyo ilisema.
''Tunaomba radhi kwa tukio hilo la kipekee la hapo jana na sasa tumeanza kuweka mikakati dhabiti ya kuzuia marudioa ya ajali hiyo'' taarifa hiyo ya KenGen ilielezea.
Mashirika mengi pamoja na wawekezaji wa kibinafsi walilazimika kufunga biashara zao hapo jana huku wale waliokuwa na nitambo binafsi za kuzalisha umeme wakiingia gharama zaidi ya kununua mafuta .
Wakenya wengi waliopokea habari hizo waliikejeli kampuni hiyo ya kuzalisha umeme wengi wakiwatania katika mitandao ya kijamii.

KISHEY PLATNUMZ!

Tuesday, June 7, 2016

Entertainment Picha,Jumba lililotumika kuhifadhi mwili wa bondia Muhammad Ali linavyolindwa.

HAYATI MOHAMAD ALI
Jumba lililotumika kuhifadhi mwili wa bondia Muhammad Ali limeonekana kulindwa vikali na timu ya askari tofauti.

Mashaidi mjini Louisville, Kentucky wameona zaidi ya magari matatu ya polisi nje ya jumba hilo la A.D. Porter & Sons. Askari hao ni kutoka kikosi cha Jefferson County Sheriff na Louisville Metro PD.

Msemaji wa nyumba hio ya kuhifadhi maiti amesema polisi wapo hapo kuzuia fujo kutoka kwa mashabiki na wapenzi pamoja na kulinda mwili wa bondia huyo.

Muhammad Ali anazikwa ijumaa hii.

Friday, June 3, 2016

Ronaldinho kutokea kwenye filamu mpya ya Van Damme

Staa wa soka duniani, Ronaldinho Gaucho amekubali kucheza kwenye filamu mpya ya kikckboxer ‘Retaliation’ ya Jean-Claude Van Damme.

RONALDINHO AKIWA ON SET
   
Ronaldinho ambaye kwenye filamu hiyo ametumia jina la Ronaldo atakuwa pamoja na mastaa wengine kama Mike Tyson, Fabricio Werdum na Paige Van Zant.
Producer Rob Hickman kutoka Hollywood amesema, “As producers, much like advertisers and brands, we must look at a potential star’s total value. In addition to his charisma, Ronaldinho also brings with him 66 million social media followers from all parts of the globe. Those numbers are an element that a lot of traditional movie stars can’t offer and when we market the film, that is something that will be invaluable.”

 Jiunge na kishey Platnumz sasa!

Friday, May 27, 2016

M 2The P aeleza kilichotokea siku Ngwea anafariki, adai anahisi kuna mkono wa mtu

Msanii wa muziki M 2The P ambaye alikuwa rafiki mkubwa wa msanii Albert Mangwea, amesema hadi leo anahisi kuna mtu aliyehusika na kifo cha Ngwea, na kumfanya ashindwe kuamini ni ajali ya kawaida.

MSANII M 2THE P AKIWA NA HAYATI NGWAIR

Akiongea katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio Ijumaa hii, M2The P amesema kitendo cha kuibiwa vitu vyao vyote ndio kilichompa wasi wasi.
“Unajua ile siku tuli-party sana,” alisema M2 The P. “ Tumepiga bata lakini kilichonishtua, ni sawa tukio lilikuwa kama ilivyoonekana ila kilichonishangaza ni baada ya kurudi ghetto tukakuta vitu vyote vimeibiwa, kitu kilichonishtua, ina maana ilikuwa ni kama walitu-target kabisa,”
Pia msanii huyo ambaye naye siku ya tuko hakuwa katika hali nzuri baada ya kupoteza fahamu, amesema kulingana na hali hiyo, anaunga mkono kauli ya mama mzazi wa Ngwea Bi. Denisia Constantino, kwamba huenda kuna watu walishiriki kusababisha kifo cha Ngwea.

Friday, May 20, 2016

Diamond kwenye headlines nyingine na Wizkid, AKA, Drake, Beyonce na Rihanna

   
   
May 20 2016 Tanzania imeamka na habari nyingine njema za Diamond Platnumz kuchaguliwa tena kushiriki kwenye tuzo za kituo maarufu cha TV Marekani kiitwacho BET ambapo Platnumz amekua na mwaka mwingine mfululizo wa kuwa nominated na sasa ni kwenye tuzo za BET Awards 2016.
Diamond ameshukuru kwa kuchaguliwa kuwania tuzo kwenye kipengele cha Best international Act Africa ambapo ameyaandika maneno haya baada ya kufikiwa na taarifa >>> ‘Ningependa niwashukuru kwa Sapoti kubwa Manayozidi kunipa na niwajuze kuwa kijana wenu nimechaguli kuwania tunzo ya Msanii Bora wa Kimataifa toka Africa kwenye tunzo za BET #BETAwards America’
Tuzo za BET 2016 ambazo zitatolewa nchini Marekani zimeanza kuchukua nafasi kwenye headlines baada ya kutangazwa list ya waliochaguliwa kuwania huku Beyonce, Rihanna na Drake wakitangazwa kuongoza kwa kuwania tuzo zaidi ya moja.






  BET 2

Wednesday, May 18, 2016

MANENO YA PELE: Pele asema kama yeye ni mfalme basi Messi ni Prince.

   

Trump: Ninaweza kuzungumza na Kim Jong-un

    
    
Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amesema yuko tayari kufanya mazungumzo na kiongozi wa Korea Kaskazini kuhusu mpango wa nyuklia wa taifa hilo.
“Ninaweza nikazungumza naye, Siwezi kuwa na tatizo kuzungumza naye,” Bw Trump alisema kuhusu Kim Jong-un.
Mkutano huo ungekuwa tofauti kabisa na msimamo wa muda mrefu wa Marekani kuhusu Korea Kaskazini.
Hatua hiyo imemfanya mgombea anayeongoza katika kinyang’anyiro cha chama cha Democratic Hillary Clinton kumshutumu Bw Trump na kusema anashangaza kwa kuwaenzi sana viongozi wababe wan chi za nje.
Taarifa iliyotolewa na mmoja wa wasaidizi wa Bi Clinton imesema sera ya mambo ya nje ya Bw Trump usio wa maana yoyote.

>>>>Kwingineko, BBC imefahamu kwamba huenda Bw Trump akazuru Uingereza kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Marekani mwezi Novemba.
Wanadiplomasia wanatarajia ziara hiyo ifanyike baada yake kuwa rasmi mgombea urais wa chama cha Republican mwezi Julai.
Mapema wiki hii, Bw Trump alisema dalili zinaonesha huenda asiwe na uhusiano mwema sana na Uingereza.
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron na meya mpya wa London Sadiq Khan, ambaye ni Mwislamu, wamemshutumu Bw Trump kutokana na hatua yake ya kupendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani.


Tuesday, May 17, 2016

Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imeomba kutengewa Trilioni 4 kama bajeti yake ijayo


Bunge la 11 limeendelea Dodoma, na leo May 17 2016 ilikuwa ni zamu ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuwasilisha hotuba yake pamoja na kuomba kupitishiwa bajeti yake ijayo.  Kazi imefanywa na Waziri  wake Makame Mbarawa ambaye ameanza na kuzitoa changamoto za Wizara…

>>‘Katika utekelezaji wa majukumu yake Wizara inakabiliwa na changamoto mbalimbali, changamoto hizo ni pamoja na upungufu wa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo, uzidishaji wa uzito wa magari ya mizigo unaosababisha uharibifu wa barabara

Msongamano wa magari katika jiji la Dar es salaam, uvamizi wa maeneo ya Hifadhi ya Barabara na Reli, kujenga uwezo wa Makandarasi wazalendo katika kutekeleza miradi ya maendeleo, ajali za barabarani, wizi wa miundombinu ya uchukuzi kutokana na biashara ya chuma chakavu n.k
Mwisho Waziri Mbarawa akaomba fedha…>>>Katika mwaka 2016/2017, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inaomba kuidhinishiwa jumla ya Shilingi 4,895,279,317,500.00’. Kati ya fedha hizo, Shilingi 2,212,141,496,500.00 ni kwaajili ya Sekta ya ujenzi

Shilingi 2,587,333,762,000.00 ni kwa ajili ya Sekta ya Uchukuzi na Shilingi 95,804,059,000.00 ni kwa ajili ya Sekta ya Mawasiliano ‘

UNGANA NAMI KISHEY PLTNUMZ SASA!

TWITTER, FACEBOOK, INSTAGRAM

Saturday, May 14, 2016

Ice Boy kutoka ‘High Table Sound’ ya Barnaba azungumzia mipango ya muziki wake

Msanii wa muziki kutoka label ya ‘High Table Sound’ ya Barnaba, ‘Ice Boy’ amefunguka na kuzungumzia maisha yake ya muziki pamoja na mipango yake akiwa ndani ya label hiyo.


Akizungumza na Bongo5, Ice Boy amesema anaamini ‘High Table Sound’ inaweza kubadili maisha yake ya muziki.“Kwa sasa nipo kwa Barnaba, tayari nimeona wapi natakiwa kwenda na kwa njia gani,” alisema Ice Boy. Kwa hiyo naweza sema hapa kwangu ni sehemu sahihi kwangu, tayari kuna kolabo za kimataifa nimefanya, kwa hiyo mashabiki wakae mkao wa kula kuna mambo mengi mazuri yanakuja,” alisema Ice Boy.

NDANI YA MIEZI MICHACHE MSANII 2FACE IDIBIA AMESAINI DILI HILI JINGINE JIPYA..

BAHATI YA MWENZIO USIILALIE MLANGO WAZI:

 
2Face Idibia asaini dili la tatu kama balozi ndani ya miezi michache.
Hatua hiyo imekuja baada ya wiki iliyopita kupata shahada ya heshima kutoka chuo kikuu cha Igbinedioncha nchini Nigeria na kuwa msanii wa kwanza wa nchi hiyo kupatiwa tuzo ya heshima kama hiyo.
Mwaka 2016 umeonekana kuwa wa neema zaidi kwa hitmaker huyo wa ‘African Queen’ baada ya kusaini mkataba mwingine na kampuni ya simu, Partner Mobile.

Baadhi ya wasanii wa nigeria waliosaini mikataba tofauti tofauti ni Davido akisaini na Pepsi Niger, Flavour na Banky W.

MFAHAMU PABLO ESCOBAR,GOD FATHER WA MADAWA YA KULEVYA ALOACHA HISTORIA YA PEKE YAKE DUNIANI

     Ushawahi kuona mtu anajenga jela yake mwenyewe na kuiremba kisha kuchagua magereza wa kumlinda, mtu alieogopwa na wauza madawa wenzake na kuwaweka majaji, polisi na wanasiasa mfukoni kwa pesa ama vitisho. Moja ya watu wakatili aliemuondoa yoyote aliekuwa kikwazo katika njia yake akiwa na sera ya aidha ukubali rushwa au risasi za Pablo. Anaitwa Pablo Escobar a.k.a El Doctor, El Patrón,Don Pablo,El Señor, El Magico. Kila $1 aliyokua anaweka katika biashara yake alikua anapata profit OR return ya $200. Alikuwa anakusanya pesa haweki bank, anatunza ndani chini ya ardhi, juu ya dari or ukutani. Adui pekee wa hela zake walikuwa ni Panya wenye njaa kali. Kila mwaka inasemekana alikua anapoteza 10% ya faida ambayo kwa haraka haraka ni $b1, Panya

walizokuwa wanakula. Marekani na Serikali ya Colombia ilitaka Pablo akamatwe na afungwe. Akakubali but Gereza akajenga yeye. Ndani ya gereza kulikuwa ni kama 5star hôtel. Alijiwekea kila kitu, Jacuzi, Bar, Pub, TV,na vitu kibao vya thamani. Pia wanawake wakawa wanaingia na akiwa jela alikuwa ana uwezo wa kutoka na kurudi kisirisiri, coz walinzi wa gereza alikuwa anawahonga vizuri sana. Baadae, Pablo alichoka maisha ya Jela la Hôtel, anataka kurudi kitaa, akatoroka. Wakati anatoroka akachukua familia yake na walinzi wake wakakimbilia Maporini. Wakati wapo huko vichakani, mtoto akaugua ghafla na kukawa na baridi sana, ukahitajika moto unajua Pablo alochofanya? Aliwasha moto wa kutoa baridi la ugonjwa wa kwa mwanae kwa kutumia noti zaidi ya 2million dollars, ziliwasha moto mtoto aote moto kupata joto, na kupika kwa note za $2,000,000, za kibongo ni b3 na m240. Alikuwa ananunua na kutumia Rubber band za $2,500 = tsh 4,050,000 za kibongo kufungia hela zake kila mwezi, so kwa mwaka alikuwa ananunua rubber band za $30,000 = 48,600,000 kufunga tu mihela yake (hata BOT hawatumii rubber band za $2,500 kwa mwezi na haijawahi kutokea kwa mtu wala taasisi) Alinunua ndege kwa ajili ya kusafirishia hela zake tu, kila trip ndege ilikuwa inabeba $10m. Mwaka 1989, Forbes ilimtaja kama tajiri wa 7 duniani, anakadiriwa kuwa na utajiri wa $25-30b, watu wake wa karibu wanasema alikuwa anazidi hata hapo coz kwa siku alikuwa anatengeneza sio chini ya $60m, coz kwa mwezi alikuwa anasafirisha zaidi ya 80-100t USA. Na ubabe wake wote, Pablo alikuwa anaogopa sana kufa. Baada ya kutoroka Jela, serikali na jeshi la Colombia wakawa wanamtafuta Pablo, akawa-offer serikali iachane nae na atailipia serikali deni ililokuwa inadaiwa $b10 zaidi ya tirioni 18 za kibongo, ili serikali imalize deni inalodaiwa, lakini serikali ilikataa, msako wa Pablo wakakabidhiwa wamarekani na kumuua December 2/1993. Mpaka leo hongo/rushwa kubwa duniani kuwahi kutokea ni hiyo ya $10b ya Pablo kutaka kulipa deni la taifa la Colombia, 10b usd = trilioni 18.


Eti kuna sehemu Kanye West akiwepo,huruhusiwi kumtazama,ni lazima utazame pembeni.

 
Muhudumu wa chakula maarufu Mjini New Yori Stacy Adler ’50’ amefunguka juu ya kitendo alichofanyiwa wakati wa shughuli ya Kanye West na kusema nikitendo ambacho hata sahau.
Kwenye kitabu kipya cha Ina Yalof ‘Food and the City’ muhudu huyu anayefanya kazi na mastaa wengi kama Beyonce, Jay Z, Jennifer Lopez, George Clooney, Madonna amesema aliambiwa asimtazame Kanye West na kwamba wakati anapita wahudumu wote waangalie pembeni.
Stacy anasema”Watu wote maarufu wako powa sana ila wapambe wao ndio wanasumbua, niliambiwa na watu wa Kanye kuwa akipita hakuna mtu wa kumtazama, lazima uweke shingo pembeni na usimuone wakati anapita kitu ambacho kilinikera sana“.